Breaking News

Your Ad Spot

Jun 15, 2014

PICHA:SHAMRA SHAMRA ZA UFUNGUZI WA ZIFF 2014 NDANI NGOME KONGWE UNGUJA

DSC_0002
Jukwaa litakalotumika kwa masuala ya burudani kuanzia leo Juni 14 hadi 22 ndani ya Ngome Kongwe katika ukumbi wa Mambo Club linavyoonekana muda huu kwenye hatua ya mwisho kuelekea ufunguzi rasmi saa moja jioni.Picha na Zainul Mzige
Opening Night: Mandela: Long Walk to Freedom
June 14th 20:20 Old Fort Ampitheatre
Opening Night Concert:
June 14th Mambo Club
Tamaduni Music (Tanzania) followed by BODY, MIND & SOUL (Malawi)
DSC_0003
Mwandishi wa gazeti la Tanzania Daima, Andrew Chale akiwa kwenye ukumbi wa Mambo Club - Ngome Kongwe visiwani Zanzibar. Kulia ni baadhi ya raia wa kigeni wakivinjari kwenye viunga hivyo.
DSC_0009
Sehemu maalum itakayokuwa ikitoa huduma wa chakula na vinywaji.
DSC_0022
Music Coordinator wa ZIFF, Edward Lusala (mwenye t-shirt ya blue) akiongoza baadhi ya wasanii kuelekea jukwaani kwa ajili ya mkutano mfupi na waandishi wa habari waliowasili mchana huu.
DSC_0034
Afisa Mawasiliano wa ZIFF, Hassan Musa “Has T” akiwatambulisha wasanii watakaotoa burudani leo kwenye ufunguzi wa Tamasha la 17 la filamu la nchi za Majahazi ZIFF kwenye mkutano mfupi na waandishi wa habari (hawapo pichani).
DSC_0042
DJ maarufu Kahlil Jacobs-Fantauzzi kutoka Puerto Rico(kushoto) akiwaeleza waandishi wa habari (hawapo pichani) namna atakavyosugua sahani za muziki usiku wa leo. Wengine ni wanamuziki wa kundi la BODY, MIND & SOUL kutoka Malawi.
DSC_0075
Music Coordinator wa ZIFF, Edward Lusala akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kuwatambulisha wasanii watakaotoa burudani kwenye ufunguzi wa tamasha hilo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages