Breaking News

Your Ad Spot

Mar 13, 2015

MTOTO ADAIWA KUKATWA UUME DAR ES SALAAM


Deogratias mongela/Ijumaa

MTOTO aitwaye Badru Muhidin mwenye umri wa miaka miwili, amepata pigo kubwa baada ya kukatwa uume wake kimakosa na babu yake aliyekuwa amempeleka kutahiriwa kienyeji huko Mbagala jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita.

Mama mzazi wa mtoto huyo, Mwajuma Hussein ambaye ni mkazi wa Yombo jijini Dar, alisema aliishi na mwanaye peke yake bila baba yake kwani walitengana Juni mwaka jana baada ya kuishi bila kufunga ndoa kwa muda mrefu, lakini mara kwa mara alikuwa akimpeleka mwanaye nyumbani kwa wazazi wa mumewe kuwasalimia.
“Wiki iliyopita babu yake Eliyasa alimuomba ili wakakae naye kwa muda mfupi, baada ya muda mfupi walimtuma mtu akaniambia kuwa wameshamtahiri, nilishangaa sana kwa kuwa hawakunitaarifu juu ya uamuzi huo, nikaenda kumuona lakini wakawa wananikataza kumtazama sehemu za siri wakidai mila zao haziruhusu kwa kipindi cha mwezi mzima.
“Kutokana na shauku ya kutaka kuthibitisha hilo, siku hiyo nilipofika tu nilimchukua na kumtazama hilo eneo ndipo nikabaini kuwa alikuwa amekatwa katika kichwa, huenda huyo ngariba hakuwa mzoefu, kamfanyia kienyeji lakini wengine wakisema huenda walitaka kufanya mambo ya kishirikina,” alisema mama huyo.
Alisema baada ya kumkuta katika hali hiyo, alianza kuhangaika naye hospitalini kutafuta msaada, alipofika Temeke aliambiwa na madaktari.kwamba kijana wake alikatwa vibaya na hivyo analazimika kufanyiwa upasuaji ili kumnusuru.
“Madaktari watatu walimuangalia na kwa kuogopa kumuathiri zaidi, waliniambia niende Muhimbili, nimeumia sana, nahofia mwanangu akija kuwa mtu mzima atakuwa goigoi tu, asije akawa shoga baada ya kukata tamaa kwa hali iliyomtokea,  japo wanasema kwa kuwa bado mdogo huenda ile sehemu ya ngozi itaota lakini ndiyo maumbile yake yatakuwa na jeraha, hatokuwa kama wanaume wengine.”
Babu wa mtoto huyo anashikiliwa na Jeshi la Polisi baada ya kufunguliwa shauri katika Kituo cha Polisi Mbagala Kizuiani kwa madai ya ukatili kwa faili namba UKATILI WA MTOTO/MBL/RB/2251/2015 4/3/2015.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages