Breaking News

Your Ad Spot

May 19, 2015

UTETEZI WA MSHTAKIWA WA PILI , DANIEL YONA KUENDELEA KUSIKILIZWA LEO

Ushahidi wa upande wa Utetezi wa mshtakiwa wa pili, Waziri wa zamani wa Nishati na Madini, Daniel Yona kuendelea kusikilizwa leo na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, baada ya  jana mwenyekiti wa jopo la mahakimu wanaosikiliza kesi hiyo, Jaji John Utamwa kuwa na udhudu wa kikazi.
Jaji Utamwa na Jaji Samu Rumanyika walianza kusikiliza kesi hiyo wakiwa Mahakimu Wakazi Wakuu kabla ya kupanda na kuwa Majaji wa Mahakama Kuu Tanzania, ambao kwa sasa wako, Kanda ya Tabora.
Kesi hiyo iliahirishwa jana na jopo la mahakimu wawili Rumanyika na Hakimu Mkazi Mkuu, Saul Kinemela.
Pande zote mbili ziliridhia sababu hiyo na kesi hiyo itaendelea kusikilizwa utetezi wa Mshtakiwa wa pili Yona, hapo leo.
Washtakiwa wengine ni, Waziri wa zamani wa Fedha, Basil Mramba na Katibu Mkuu wa zamani wa Wizara ya Fedha, Gray Mgonja wote wanakabiliwa na kosa la matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia Serikali hasara ya Sh. bilioni 11.7 kwa kutoa msamaha wa kodi kwa Kampuni tanzu ya Alex Stewart ( ASSAYERS) Government Business Corporation.
Katika kesi ya msingi, washtakiwa wanadaiwa kuwa, kati ya Agosti mwaka 2002 na Juni 14 mwaka 2004 jijini Dar es Salaam, wakiwa watumishi wa umma kama mawaziri na katibu mkuu walitumia vibaya madaraka.
Ilidaiwa kuwa kwa kupitia kampuni ya Alex Stewart (ASSAYERS) ya Uingereza iliyoingia mkataba wa ukaguzi wa madini ambapo kwa kupitia kampuni tanzu ya Alex Stewart ( ASSAYERS) Government Business Corporation waliingia mkataba kukagua kiwango cha uzalishaji wa madini ya dhahabu kinyume cha Sheria ya Manunuzi ya Umma.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages