Breaking News

Your Ad Spot

Jun 14, 2015

SITTI MTEMVU ALIVYOBADILISHA MAUMIVU YA SIKU 30 KUWA BIASHARA

Aliyewahi kuwa waziri mkuu wa Uingereza kuanzia mwaka 1940 hadi 1945 na kisha kurejea tena mwaka 1951 hadi 1955, Winston Churchill aliwahi kusema, “a pessimist sees the difficulty in every opportunity; an optimist sees the opportunity in every difficulty.”
Alimaanisha kuwa “mtu muoga huona ugumu kwenye kila fursa na mtu jasiri huona fursa kwenye kila ugumu.”
2014 ulikuwa ni mwaka wenye majaribu na mitihani mingi kwa Sitti Mtemvu.Mara tu baada ya kushinda taji la Miss Tanzania 2014, skendo moja baada ya nyingine zikaanza kuibuka. Kubwa lilikuwa ni kitendo chake cha kudaiwa kudanganya umri na kuwasilisha cheti cha kuzaliwa ‘feki.’
Pia watu wakazusha kuwa mrembo huyo ana mtoto, kitu ambacho ni kinyume cha vigezo vya shindano hilo lililofungiwa mwaka jana.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages