Breaking News

Your Ad Spot

Jun 14, 2015

MKUU WA WILAYA YA KINONDONI AZINDUA TAMASHA LA MICHEZO

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Paul Makonda  Amezindua Tamsha la Michezo na afya lenye lengo la kuboresha afya ambalo limeandaliwa na kampuni ya Fern (T) Ltd Lililofanyika leo 14 katika viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam.Lengo kubwa la tamasha hilo ni kuwakutanisha watu wa rika mbalimbali ili kufurahia na kuweka miili yao sawa kwa afya bora.Tamasha hilo Limepambwa na burudani kwa ajili ya kuwaburudisha watu na wataalamu mbalimbali waliobobea kwenye sekta ya ufundishaji juu ya ufanyaji mazoezi na wataalamu wa afya watakuwepoa kwa ajili ya kutoa ushauri wa afya na lishe.
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Paul Makonda  Akiteta Jambo na Mratibu wa tamasha hilo, Dimo Debwe Mitiki.Katika jitihada za kuijengea jamii ya kitanzania tabia ya kufanya mazoezi kwa ajili ya kuboresha afya zao, kampuni ya Fern (T) Ltd Iliona ni vema Kuandaa  tamasha la kimichezo lililoambatana na mazoezi pamoja na burudani kwa ajili ya watu wa kada mbali mbali.
 Lengo kubwa la tamasha hilo ni kuwakutanisha pamoja watu wa kariba mbalimbali na umri tofauti kufurahi pamaja na kuweka miili yao fit na kuongeza kuwa, watakuwepo wataalamu mbalimbali waliobobea kwenye sekta ya ufundishaji juu ya ufanyaji mazoezi na wataalamu wa afya watakaotoa ushauri mbalimbali wa afya na lishe.
 
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Paul Makonda Alipata nafasi ya Kupima Afya yake kwenye Tamasha hilo kutoka kwa Wataalamu wa Afya na Lishe walioendesha zoezi hilo bure..Kwa siku za hivi karibuni watu wengi wamekuwa wakifuatilia sana masuala ya afya kitu ambacho kimepelekea kuibuka kwa vikundi vingi/vilabu vingi vya mazoezi. Kutokana na kutokuwepo kwa muundo rasmi unaowakutanisha watu hawa wapenda mazoezi Fern imetambua na kuona fursa hiyo kupitia Tamasha Hilo..
  Washiriki wa Tamasha hilo Kutoka maeneo Mbalimbali ya Mkoa wa Dar es Salaaam  wamepata Nafasi ya Kufanya Mazoezi ya Jogging Pamoja na Mkuu wa Wilaya.Washiriki wa tamasha hilo kuwa ni pamja na Joging clubs zaidi ya 100 kutoka wilaya zote 3 za mkoa wa Dar es Salaam; Temeke,Kinondoni na Ilala, makampuni na Taasisi mbalimbali wakiwemo, CRDB Bank, TCDC, SMART TELECOMMUNICATION, PSI ,washiriki wengine ni pamoja na Gyms kama vile AZURA, THE GYM, GENESIS HEALTH CENTRE, POWER ON FITNESS, HOME GYM NA UNIVERSAL GYM, wasanii wa tasnia ya Filamu na Muziki nchini.Wahiriki walikusanyika viwanja vya leaders kuelekea Coco beach na kuzunguka maeneo ya kinondoni kisha kurudi tena Leaders na baada ya watu kurudi leaders waliendelea na mazoezi ya viungo
Zoezi hili likimalizika litafuatiwa na kipindi cha dondoo za lishe na afya kutoka kwa kwa wataalamu waliobobea ambapo watu watapata fursa wa kujifunza mambo kadhaa yahusuyo afya,” alifafanua 
 Tamasha hilo lililokuwa la aina yake limewavutia watu mbalimbali
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Paul Makonda Akiongea na Mmoja wa Watoto walioshiriki Tamasha hilo leo
 
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Paul Makonda Akishiriki Kufanya Mazoezi Mbalimbali Katika Tamasha hilo lililofanyika Katika Viwanja vya Leaders

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages