Breaking News

Your Ad Spot

Jun 9, 2015

TBL YAPATA USHINDI WA USALAMA NA USAFI WA MAZINGIRA


 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Raymond Mushi (kushoto), akikabidhi Cheti cha ushindi wa kwanza kwa Meneja Usalama na Mazingira wa kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Renatus Nyanda, kutambua mchango wa TBL kutunza mazingira, wakati wa kilele cha Wiki ya Mazingira, iliyofanyika Dar es Salaam hivi karibuni.

 Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), baada ya kushiriki katika zoezi la usafi wa mazingira katika soko la Mchikichini, Dar es Salaam

 Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi (kushoto) akishirikiana na wafanyakazi wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), katika soko la Mchikichini, Dar es Salaam jana, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya mazingira, ambapo TBL imesaidia vifaa mbalimbali vya usafi kwa Manispaa ya Ilala. Kulia ni Meneja wa Kiwanda hicho, Bw. Calvin Martine.

 Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi (kushoto) na Meneja wa Kiwanda cha Bia Tanzania (TBL), Bw. Calvin Mushi wakisukuma toroli zenye  takataka, baada ya kufanya usafi katika soko la Mchikichini, Dar es Salaam jana, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya mazingira, ambapo TBL imesaidia vifaa mbalimbali vya usafi kwa Manispaa ya Ilala.



 Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi (kushoto) akimuaga Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Dorris Malulu baada ya kushiriki katika maadhimisho ya wiki ya usafi katika soko ya Mchikichini Dar es Salaam jana, ambapo TBL imesaidia vifaa mbalimbali vya usafi kwa Manispaa ya Ilala. Kulia ni Meneja wa Kiwanda cha Bia Tanzania Bw. Calvin Martine.



 Baadhi ya wafanyakazi wa Manispaa ya Ilala wakishiriki usafi katika soko la Mchikichini, Dar es Salaam jana, baada ya Manispaa hiyo kupewa vifaa mbalimbali vya usafi vilivyotolewa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya Mazingira.



Baadhi ya wafanyakazi wa Manispaa ya Ilala wakishiriki usafi katika soko la Mchikichini, Dar es Salaam jana, baada ya Manispaa hiyo kupewa vifaa mbalimbali vya usafi vilivyotolewa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya Mazingira.


No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages