Breaking News

Your Ad Spot

Nov 29, 2015

MBUNGE WA JIMBO LA ILALA MSSA ZUNGU ATEKELEZA AHADI ALIYOITOWA WAKATI WA KAMPENI

  Mbunge wa Jimbo la Ilala Mussa Zungu (CCM) (mwenye kofia) akimkabidhi nahodha wa timu ya Ferry Beach Boys, Selemani Ally 'Kaseja' nyaraka za  Pikipiki hiyo Dar es Salaam leo ambayo ilikuwa ni moja ya ahadi yake kwa kikosi hicho wakati wa kampeni.(PICHA NA  KHAMISI MUSSA)
 Mbunge wa Jimbo la Ilala Mussa Zungu (CCM) (mwenye kofia) akimkabidhi nahodha wa timu ya Ferry Beach Boys, Selemani Ally 'Kaseja' namba ya Pikipiki Dar es Salaam leo.  

 Zungu amesema  ilikuwa ni moja ya ahadi yake kwa kikosi hicho wakati wa kampeni alipofika kituoni hapo wakati alipopita kumuombea kura aliyekuwa mgombea  Urais Mgufuli  kupitia Chama cha Mapinduzi  CCM  ili iwasaidie kujikusanyia kipato kwa njia hiyo ya kujikusanyia kipato ili wapate nauli wanapokuwa wakienda kucheza kwenye pindi wapatapo mwaliko,   Mbunge huyo aliendelea kusema nitaendelea kusaidia maswala ya timu na alipewa ombi la timu kusaidia vifaa vya michezo  lakini leo nakusaidieni Pikipiki iwe mali ya timu si mali ya mtu, anaendelea kusema Zungu, alitowa ahadi ya Bodi ya Ferry na bodi hiyo ipo tayari  tunasubiri waraka uchapishwe na fikiri kabla ya mwezi wa kumi na mbili kwisha bodi itakuwa imeundwa ili Soko hili liendeshwe na wafanya Biashara wenyewe, na niliweka ahadi ya kuwawekea mahema kwenye maeneo ya wanaouza Samaki maeneo ya wanaopigwa na Juwa na kabla ya mwezi wa kumi na mbili itakuwa tayari.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages