Breaking News

Your Ad Spot

Nov 27, 2015

SERIKALI YA AWAMU YA TANO "MOTO", DKT. MAGUFULI AMSIMAMISHA KAZI BOSI WA TRA, WAZIRI MKUU NAYE AAMURU MAAFISA KADHAA WAKAMATWE


Na K-Vis Media
SERIKALI ya awamu ya tano chini ya uongozi wake Rais wa jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli imekunjua “makucha”, ambapo leo Ijumaa Novemba 27, 2015 Rais Dkt. Magufuli amesimamisha kazi Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, TRA Bw.Rished Bade kufuatia ziara ya kushitukiza ya Waziri Mkuu Bw. Kassim Majaliwa mapema leo asbhi pale Bandari ya Dar es Salaam.
Waziri Mkuu Majaliwa, alibaini kupitishwa bila ya kulipiwa ushuru makontena 349 yenye bidhaa na kusababisha hasara ya zaidi ya shilingi bilioni 80.
Kufuatia “Madudu hayo” Waziri Mkuu aliagiza wale woooote waliohusika au wanaohusika na uhakiki na ruhusa ya makontena hayo, wakamatwe mara moja.
Baada ya uamuzi huo, majira ya Alasiri ya leo Ijumaa Novemba 27, 2015, Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli naye aliona hatua hiyo lazima iongezwe nguvu na kutangaza kumsimamisha kazi mara moja Kamishna huyo Mkuu wa TRA.
na nafasi yake kukaimiwa na Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Dkt Philip Mpango.
Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, iliyotolewa na Ikulu ya Rais imesema, uteuzi huo unaanza mara moja na wale woote waliotajwa kwenye kashfa hii ya sasa, hawataruhusiwa kusafiri nje ya nchi hadi pale uchunguzi dhidi yao utakapokamilika.
 

 Dkt. Philip Mpango, Kaimu Kamishna Mkuu wa TRA
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli
Hii ndiyo bandari ya Dar es Salaam, ambayo kwa muda mwingi imekuwa ikihujumiwa na kutoa mapato yasiyolingana na ukubwa na utendaji wake wake

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages