Watu wenye silaha wamewapiga risasi na kuwauwa watu 9 usiku wa kuamkia leo katika mji mkuu wa Burundi- Bujumbura
Watu
hao waliokuwa katika kilabu cha burudani mjini Bujumbura waliamrishwa
walale chini kabla ya kufyatuliwa risasi na kuuawa papo hapo.
Meya wa mji huo ametaja kisa hicho kama mauwaji ya kinyama.
Waliwauawa 7 na kuwajeruhi wengine wawili alisema Freddy Mbonimpa meya wa mji huo.
Mauaji hayo yanatukia katika siku ya mwisho iliyotolewa na serikali
kwa raia walioko na silaha kuzisalimisha kwa vyombo vya dola.
Awali
Serikali ilikuwa imewapa watu fursa ya kusalimisha silaha walizo nazo
lau sivyo polisi wachukue hatua kali dhidi yao kuwapokonya.
Hapo
jana wenyeji wa vitongoji vya mji wa Bujumbura walionekana wakitoroka
makwao kwa hofu ya makabiliano na vyombo vya serikali.
Mwandishi
wa BBC mjini Bujumbura, aliwaona watu wamebeba magodoro na kadhalika
katika mabarabara, wakihamia kwenda kwa marafiki na jamaa katika mitaa
salama.
Watu zaidi ya laki mbili wamekimbilia nchi za nje.
Katika juma lilopita pekee , watu 13 wamekufa, hasa kwenye mitaa ambako upinzani una nguvu.
Idadi
ya watu waliouawa sasa imegonga 22 na kuongeza idadi ya awali ya watu
200 ambao wameuwawa katika wimbi la machafuko ya kisiasa nchini humo,
tangu mwezi Aprili, pale rais Pierre Nkurunziza alipotangaza nia ya
kuwania tena kiti cha urais kwa muhula wa tatu.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269