Waziri wa
Kilimo,Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba amewahakikishia wananchi
kuwa serikali ya awamu ya tano ya Rais John Magufuli imejipanga kutetea
haki za wananchi na itamuwajibisha yeyote anayehujumu kilimo na ustawi
wa Taifa.
Waziri
Nchemba amesema hayo katika ziara yake anayofanya katika mikoa ya
Morogoro na Iringa katika maeneo mbalimbali ya wakulima na mashamba ya
wananchi na wadau wengine katika sekta hiyo.
Wizara
inajipanga kuandaa mfumo mzuri wa kuhakikisha kila mwananchi anafikiwa
kupata pembejeo kwa wakati na upatikanaji wake uwe rahisi.
Lakini,Mwigulu
Nchemba pia amewasihi sana wawekezaji kwenye mashamba n.kuheshimu
taratibu za uwekezaji,ili kuondoa mahusiano mabaya kati ya muwekezaji na
wananchi.Mwisho,Mh.Mwigulu Nchemba anaendelea na ziara yake ya kukagua
vituo vya utafiti, Mashamba ya mbegu na,Mifugo na uvuvi katika Mkoa wa
mbeya kuanzia tar.5/03/2016.
Waziri wa
Kilimo,Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba akiteta jambo na Mbunge wa
Mlimba Bi suzan Kiwanga (CHADEMA) mapema hii leo wakati wa mkutano wa
hadhara uliofanyika kijiji cha Mgeta-Mlimba.Pichana Festo Sanga
Waziri wa
Kilimo akipewa maelezo kuhusu uhudumiaji wa mashamba ya Mahindi kuanzia
uaandaji wa shamba, mbegu,mbolea na majira ya kupanda mahindi.Wakati wa
ziara hiyo, Mwigulu Nchemba mwenye dhamana ya kilimo ameendelea
kusisitiza kuwa kuna haja kama Taifa kuachana na kilimo cha jembe la
mkono,lakini matumizi ya mbegu bora na mbolea bora ni muhimu
yazingatiwe.
Mwigulu
akiangalia sehemu ya mpunga uliohalibiwa kwa kile kinachodhaniwa ni
sumu iliyotokana na Umwagiliaji wa sumu aina ya Glyphosate iliyokuwa
inatumiwa na wamiliki wa KPL kuchoma nyasi kwenye mashamba yao,Katika
kikao cha pamoja cha wananchi,Uongozi wa serikali na uongozi wa
KPL(Kilombero Plantation Limited), Mwigulu Nchemba amepokea hatua za
awali za wataalamu na watafiti wa serikali waliobobea kubaini chanzo cha
mimea kuharibika kwa kiasi kikubwa hivi,Wataalam hao wamemhakikishia
Mh.Mwigulu Nchemba kuwa watatoa ripoti yao kamili ndani ya muda wa siku
21 ili kubaini aliyesababisha mimea ya mpunga kuungua.
Moja ya
mashine za Umwagiliaji kwenye mashamba ya Mpunga ya KPL(Kilombero
Plantation Limited) ikiwa tayari kwa kuanza kazi ya kumwagilia maji
kwenye shamba hili la mpunga.
Moja ya trekta la kisasa la muwekezaji wa “Ruaha Farm” ambalo linatumika kupanda mbegu,kuvuna na mwagilia dawa ya mimea.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269