Breaking News

Your Ad Spot

Jul 13, 2016

RAIS DK. MAGUFULI AZINDUA LEO MPANGO WA UGAWAJI MADAWATI KWA MAJIMBO MBALIMBALI NCHINI, AWATAKA JKT, MAGEREZA KUKAMILISHA HARAKA MADAWATI YALIYOSALIA

 Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akimuonesha Rais Dkt. John Pombe Magufuli sehemu ya Madawati yaliyotengenezwa na fedha zilizopatikana kutokana na kubana matumizi kutoka Ofisi ya Bunge katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua Madawati hayo yaliyotengenezwa na Jeshi la Magereza pamoja na Suma JKT
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amekaa kwenye moja ya Dawati katika hafla hiyo fupi ya ugawaji wa Madawati hayo.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Mwanafunzi wa darasa la tano katika shule ya Msingi Bunge George Samwel wakati akiangalia mfano wa darasa ya jinsi madawati hayo yatakavyo katika katika shule mbalimbali nchini.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Wanafunzi wa Shule ya Msingi Bunge wakwanza kulia Mariam Elias (darasa la tatu na wapili kutoka kushoto George Samwel mwanafunzi wa darasa la tano wakiwa wanapiga makofi kabla ya tukio la ugawaji wa madawati hayo yaliyotokana na kubana matumizi kutoka Ofisi ya Bunge.
 Mwanafunzi wa darasa la tano katika shule ya Msingi Bunge George Samwel akimtajia Mheshimiwa Rais Jina la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mara baada ya kumuuliza huku Waziri Mkuu akitazama kwa furaha.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi Mbunge wa Ilala Mussa Azzan Zungu ambaye aliyapokea kwa niaba ya Wabunge wa majimbo mbalimbali nchini.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ndogo ya Tume ya huduma za Bunge inayoshughulika utengenezaji wa madawati. Waliosimama mbele ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa, Naibu Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson, Mbunge wa Ilala Mussa Azan Zungu pamoja na Waziri wa Ulinzi Dkt. Hussein Mwinyi.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Wanafunzi wa Shule ya msingi Bunge mara baada ya tukio la kukabidhi madawati katika Majimbo mbalimbali nchini. Wengine katika picha ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson pamoja na Waziri wa Elimu Prof. Joyce Ndalichako
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia baadhi ya Maaskari brass bendi ya Jeshi la Magereza mara baada ya kukabidhi Madawati
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Bunge katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Mwanafunzi wa Darasa la tatu katika Shule ya Msingi Bunge Mariam Samwel wakati akiondoka kwenye viwanja hivyo 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli  akisalimiana na Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa aliyehudhuria hafla hiyo ya ugawaji wa Madawati katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU. HABARI KAMILI>>BOFYA HAPA

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages