Breaking News

Your Ad Spot

Jul 15, 2016

WATU 80 WAUAWA KATIKA SHAMBULIO LINALODHANIWA KUWA LA KIGAIDI NCHINI UFARANSA



NA K-VIS MEDIA/NA MASHIRIKA YA HABARI
KWA uchache watu 80 wameuawa na wengine 18 wamejeruhiwa vibaya katika shambulio la kigaidi mjini Nice Ufaransa usiku wa kuamkia Julai 15, 2016.
Taarifa za vyombo vya habari zinasema, washambulizi walitumia lori, kuvamia umati wa watu waliokuwa wakisherehekea Bastille Day kwenye mji wa Nice Kusini mwa Ufaransa.
Gazeti la Nice Matin lilimnukuu mwandishi wake aliyeko eneo la tukio akisema, watu wengi wamejeruhiwa na damu imetapakaa kwenye mitaa.
Silaha nyingi zilikutwa kwenye lori hilo na dereva wake ametambuliwa kuwa ni mkazi wa mjini humo mwenye asili ya Tunisia.
Rais wa Ufaransa Francois Holand, amesema shambulio hilo lina harufu ya ugaidi.
“Tuko kwenye vita dhidi ya magaidi, wanaotaka kutuumiza kwa gharama yoyote.” Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ufaransa, Bernard Cazeneuve amesema.





No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages