Breaking News

Your Ad Spot

Nov 25, 2016

KAMATI YA ULINZI MKOA WA KIGOMA YABAINI UHARIBIFU WA MAZINGIRA MSITU WA MAKERE-KASULU


NA MAGRETH MAGOSSO,KIGOMA

IMEFAHAMIKA ,kuwa shughuli za kilimo,ufugaji holela,uchomaji wa mkaa na uchimbaji wa madini ya Chokaa katika Hifadhi ya Msitu wa Makere Kusini uliopo Halmashauri ya wilayani kasulu Mkoa wa Kigoma ni chanzo cha mabadiliko ya tabia Nchi  .

Shughuli hizo zimebainika kukithiri katika hifadhi hiyo,juzi baada ya Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa kwa kushirikiana na kamati ya wialani humo,kutembelea hifadhi hiyo,ili kujionea uharibifu mkubwa uliofanywa na wananchi kwa kushirikiana na wahamiaji haramu kutoka nchi jirani, kujikita katika shughuli  hizo,kinyume cha sheria na taratibu za Nchi,ambapo hufanya hayo katika vyanzo vya maji na kitendo cha kukata miti hovyo ni janga la ukame na mafuriko siku za usoni.

Meneja wa Misitu wilayani humo Donald Silaha alisema licha ya uongozi wa wilaya kutoa agizo rasmi la wananchi waliovamia eneo hilo waondoke mara moja lakini changamoto ya kutoka ni sugu kwa walengwa kwa kuwa wanadhani maisha yapo katika msitu huo,bila kujali athari ya mabadiliko ya tabia nchi kwa leo na kizazi kijacho.

Silaha alifafanua kuwa kushindwa kwa idara kuwajibika kikamilifu inachangiwa na ukosefu wa vitendea kazi hasa gari la doria,mafuta na uchache wa watumishi katika sekta hiyo nyeti ,kwa kuwa serikali imeajili watu wachache na uhalisia wa jiografia ya wilaya ya kasulu ukiwemo msitu wa makere ni tete kutokana na ukubwa wa msitu ,uharibifu uliofanywa ni mkubwa mno na uvamizi ni mkubwa ilihali watumishi haba.

Akikaimu nyadhifa ya Mkuu wa wilaya ya Kasulu ,mkuu wa wilaya ya Buhigwe Kanali Malko Gaguti alisema kila kukicha,wananchi hawataki kutoka katika msitu wa makere kutokana na rutuba iliyopo,bila kupima athari ya uvamizi katika msitu huo ambao unakatwa miti kila kukicha kwa ajili ya shughuli za kilimo,uchimbaji chokaa huku wafugaji wakimaliza uoto wa asili kutokana na mifugo kulishwa humo.

Mrakibu  msaidizi idara ya uhamiaji wilayani humo Emanuel Mpoyo aliongeza kwa kubainisha idadi ya wahamiaji waliowakamata katika shughuli hizo ni 700,kitendo kinachochangiwa na wananchi wa humo kushirikiana nao katika uvamizi wa hifadhi yam situ huo.

Akihitimisha hilo Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Brigedia Mstaafu Emanuel Maganga aliagiza kamati hizo zitumie kila njia kuhakikisha wanadhibiti uvamizi holela wa wakulima,wafugaji  katika msitu huo ambao ni hazina kwa wilaya ya kasulu lakini wanaharibu katikati yam situ huku nje msitu ukionekana mzuri ilihali ndani ni jangwa kwa kuwa miti huvunwa kwa shughuli za uchomaji mkaa,kilimo,ufugaji na uchimbaji wa madini.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages