Serikali ya Burundi imekana kwamba inakiuka
haki za binadamu licha ya kuendelea mwenendo wa kutoweka raia nchini
humo katika mazingira ya kutatanisha.
Hayo yamesisitizwa na maafisa wa serikali ya Burundi baaada ya
jjumuiya mbalimbali za kutetea haki za binadamu hususan shirika la Iteka
kutangaza kuwa, serikali ya Bujumbura inatumia siasa za kueneza woga na
hofu baina ya wananchi na kwamba mwenendo wa kuuawa na kutoweka raia
bado unaendelea.
Taasisi za kutetea haki za binadamu nchini Burundi zinasema kuwa,
kumeripotiwa kesi nyingi za kutiwa nguvuni wapinzani wa serikali na
baadaye kutoweka kabisa na kwamba watu wengine wanashindwa kutoka nje ya
makazi na nyumba zao.
Gaston Sindimwo, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Burundi, amekanusha
ripoti hiyo akisema kuwa, baadhi ya wapinzani wanaobeba silaha
wanavuruga amani na nidhamu na kwamba watu kama hawa wanafikishwa
mahakamani na kuchukuliwa hatua za kisheria.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269