Breaking News

Your Ad Spot

Sep 13, 2017

DC KILOLO AWATAKA WAZAZI KUWASOMESHA WATOTO WAO

Mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abdallah akiwa katika ziara ya kuzitembelea shule za msingi za kata ya Bomalang'ombe  na kujionea jinsi gani shule hizo zinavyoongozwa na kuzitambua changamoto zinazowakabili walimu,wanafunzi,wanachi na viongozi wanaozizunguka shule hizo lengo likiwa ni kuboresha utoaji wa elimu bora kwa wanafunzi wa wilaya ya kilolo.

Mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abdallah akizungumza na baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Bomalang'ombe.

Na Fredy Mgunda,Iringa

Wanachi wa kijiji cha mwatasi wamekuwa kikwazo cha wanafunzi kufanya vizuri katika masomo ya shule ya msingi kutokana na wazazi kutowatimizia mahitaji muhimu watoto wao pindi waendepo shule.

Akizungumza na waandishi wa habari waliofika katika shule hiyo mwalimu mkuu wa shule ya msingi mwatasi Seth Mfikwa alisema kuwa wazazi wengi wa kijiji hicho wamekuwa kikwazo cha maendeleo ya wanafunzi kwa kuwakatisha tamaa juu ya umuhimu wa elimu.

“Hapa kijijini wazazi wengi hawapendi watoto wao kwenda kusoma kwa kuwa watakuwa wanapunguza nguvu kazi zao mashambani ndio maana hawawapatii mahitaji muhimu ya kuwasaidia wanafunzi kusoma kwa uhuru” alisema Mfikwa

Mfikwa alimuomba mkuu wa wilaya ya kilolo Asia Abdallah kutafuta wataalam wa saikolojia kuja kuwapa elimu wazazi wa kijiji cha Mwatasi ili kukuza taaluma kwa wanafunzi wa kijiji hicho.

“Ukiangalia hali ya ufaulu wa shule hii sio mzuri kutokana na wazazi kutokujua umuhimu wa elimu lakini tunaendelea kuwaelimisha kidogo kidogo hivyo kwa kuwa mkuu leo umefika kwenye shule yetu tunaomba msaada wako wa kutoa elimu kwa wazazi ili kukuza elimu kwa wanafunzi wa kijiji hiki” alisema Mfikwa.

Aidha Mfikwa alisema kuwa wamekuwa wakiitisha mikutano ya mara kwa mara lakini bado tatizo kubwa hivyo jitihada zinahitajika kukomesha tabia hiyo kwa kuwa bila hivyo watoto wa kijiji hichi wataendelea kuwa wafanyakazi za ndani tu.

Anderson Mdeke ni diwani wa kata ya Bomalang’ombe alikiri kuwa wazazi wa kijiji cha mwatasi hawana elimu juu ya umuhimu wa kujua dhamani ya elimu katika maendeleo ya familia zao na taifa kwa ujumla.

“Kweli kabisa wazazi wa kijiji cha mwatasi wamekuwa wakiwaambia watoto wasifanye mitihani vizuri ili wasifaulu kwa kuwa wakifaulu watakuwa na gharama kubwa ya kuwasomesha hivyo wakifeli wataenda kuwafanya kazi za ndani na dio furaha kwa wazazi wa kijiji cha Mwatasi” alisema Mdeke

Mdeke alisema kuwa uongozi wa kata ya bomalang’ombe utaendelea kutoa elimu kwa wazazi hao ili kurudisha morali ya kuendelea kuwapa mahitaji muhimu yanayohitajika shuleni kwa kwa lengo la kuboresha maisha ya watoto hao.

“Zana potofu zimekuwa kikwazo kikubwa sana katika maendeleo ya wananchi wa kijiji cha Mwatasi hivyo tukiondoa zana hiyo elimu itakuwa kwa wanafunzi wa kijiji hichi” alisema Mdeke

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abdallah aliahidi kulifanyia kazi tatizo hilo kwa kuzungumza na wazazi ili kuwaelimisha juu ya umuhimu wa elimu kwa wananchi wa kijiji hiki cha Mwatasi.

“Tangu nianza ziara katika wilaya ya kilolo leo ndio nimekutana nah ii changamoto ya wazazi kuwarudisha nyuma kielimu hivyo nitatenga muda muafaka wa kuja kuongea na wazazi wa kijiji cha Mwatasi kwanza swala hili limenishtua sana kwakweli lazima nilitafutee ufumbuzi haraka sana”alisema Abdallah

Aidha mkuu wa wilaya hiyo Asia alisema anatakiwa kujifunza tabia za wananchi wa kijiji cha Mwatasi kwanini wanafanya hivyo kwa kuwa changamoto hiyo ni kubwa na inatakiwa kutatuliwa mapema.

“Unajua lazima nijue chanzo cha kuwakatisha tamaa watoto wao wasiendelee na masomo ni nini hivyo nikijua tatizo ni nini naweza kutatua tatizo hilo kwa urahisi kabisa maana elimu ni kitu mhimu sana kwa maendeleo ya watoto yao” alisema Abdallah 

Abdallah alisema licha ya changamoto hiyo ya wazazi hata walimu wa shule wanamatatizo kwani haiwezekani kuwa na walimu wengi hivi lakini ufaulu bado upo chini lazima kukaa chini na hawa walimu kujua tatizo ni nini.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages