Breaking News

Your Ad Spot

Jun 21, 2014

Baadhi ya wakazi wa jiji la Dar es salaam wamejitokeza kuanzisha mfuko maaluum wa kuwasaidia wafanyabiashara wapatao 5700 wa soko la Mchikichini walioathiriwa na janga la moto lililotokea usiku wa kuamkia tarehe 12 mwezi huu eneo la Karume,jijini Dar es salaam.

 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam ambaye pia ni mkuu wa wilaya Ilala Bw. Raymond Mushi akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu kuanzishwa kwa mfuko wa kuwasaidia wafanyabiashara wa soko la Mchikichini walioathiriwa na janga la moto kwa lengo la kurejesha hali ya maisha waliyokuwa nayo hapo awali.
 Mmoja wa waanzilishi wa mfuko wa kuwasaidia waathirika wa moto soko la Mchikichini ambaye pia ni Meneja wa Vituo vya mizigo vya nchi kavu wa Kampuni ya AZAM Bw. Raymond Adolph akieleza namna walivyoguswa na tukio la moto lililotokea katika soko hilo na kuwaomba watanzania kuunga mkono juhudi hizo.
 Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa soko la Mchikichini Bw. Jumanne Kongolo akiongea na waandishi wa habari  kuishukuru serikali na wananchi waliojitokeza kufungua mfuko wa kuwasaidia waathirika wa moto katika soko hilo.
Baadhi ya wafanyabiashara wa soko la Mchikichini walioathiriwa na janga la moto wakifuatilia masuala mbalimbali ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa mfuko wa kuwasaidia wafanyabiashara hao.Picha na Aron Msigwa –MAELEZO.
---
Na Aron Msigwa – MAELEZO,  Dar es salaam.
 Baadhi ya wakazi wa jiji la Dar es salaam wamejitokeza kuanzisha mfuko maaluum wa kuwasaidia wafanyabiashara wapatao 5700  wa soko la Mchikichini walioathiriwa na janga la moto  lililotokea usiku wa kuamkia tarehe 12 mwezi  huu eneo la Karume,jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages