Eliud (kushoto), akiwa na pacha wake, Elikana
--
Dar es Salaam na Mbeya. Daktari aliyewapokea
watoto pacha waliokuwa wameungana katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili
na kuwapeleka India kufanyiwa upasuaji, Zaituni Bokhary anatarajia
kuwasili nchini leo akitokea masomoni Misri na kwenda Mbeya kuwajulia
hali watoto hao.
Pacha hao, Elikana na Eliud walizaliwa Februari 20
mwaka jana katika Hospitali ya Wilaya ya Uyole kabla ya kuhamishiwa
Hospitali ya Rufaa ya Mbeya na baadaye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili
kutokana na kuzaliwa wakiwa wameungana kiunoni.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269