Kwa
wale watumiaji wa mtandao maarufu wa kijamii wa Twitter, bila shaka
hawatakuwa wageni wa zile akaunti ambazo zinakuwa zimethibitishwa rasmi
au kwa jina lingine Verified Account ambazo kwa kiasi kubwa humilikiwa
na watu mashuhuri kama vile marais, wasanii wa muziki, filamu na
wanasiasa.
Kwa hapa kwetu Tanzania ni baadhi ya watu wachache
waliobahatika kumiliki akaunti za namna hiyo akiwemo mkuu wa nchi Rais
Jakaya Kikwete, mbunge wa Bumbuli kupitia tiketi ya CCM Mhe.january
Makamba pamoja na msanii wa muziki wa kizazi kipya AY.
hata hivyo idadi hiyo imeongezeka tena baada ya wasanii
wawili wa muziki wa kizazi kipya wanaofanya vizuri katika gemu, hapa
namzungumzia mshindi wa Tuzo saba za Kili Diamond Platnumz na Vanessa
Mdee baada ya akaunti zao za Twitter kuwa Verified.
”What a birthday just got verified!!! Heeeey @Verified that’s wussup”
aliandika Vanessa AKA Vee Money ambaye leo anasherekea siku yake ya
kuzaliwa na kwa upande wa Diamond nae hakuwa nyuma aliandika ”Thank You Twitter” …
Happy BornDay Vee Money!!!
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269