Breaking News

Your Ad Spot

Jun 10, 2015

BI MOZA AFANIKISHA KUMPELEKA MTOTO WAKE INDIA KWA MATIBABU


Bi Moza akiwa  akimshindikiza  mtoto wake Moh'd Saidi,  Nchini India kwa matibabu Bi Moza Moh'd Khamis anapenda tena kutoa shukurani za dhati kwa wale wote waliochangia kwa hali na mali kwa mtoto wake Moh'd Said Moh'd,  kwenda kufanyiwa matibabu ya upandikizaji wa figo, nchini India.
Mapema asubuhi ya jana Bi Moza aliongea na blog ya swahilivilla ili kutoa taarifa kwa kukamilika safari yake ya kwenda nchini India pamoja na kutaka tumuombe Dua za kumtakia kila la kheri  katika safari hiyo.
Moh'd Said Moh'd ameondoka jana Jumanne Juni 9, katika  uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam kuelekea Nchini India kwaajili ya matibabu yake.
Napenda kuchukua fursa hii kwa niaba ya Tanzania Bloggers Network (DMV) na waTanzania wote waishio Nchini Marekani, kumtakia kila la kheri  Ndugu yetu Moh'd Said Moh'd katika matibabu yake huko Nchini India M/Mungu amjaalie wepesi katika safari yake na ampe afuweni na mafanikio katika mipangilio yote matibabu yake. Ameen.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages