Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani amesema kuwa Washington
na Moscow zimekubaliana kutojadili madai ya kukiuka makubaliano ya
usitishaji vita nchini Syria ambayo yalianza kutekelezwa hivi karibuni
na kuongeza kuwa vikosi vya nchi mbili hizo vitalenga tu kundi la
kigaidi na kitakfiri la Daesh na al-Nusra katika mashambulizi yao.
Katika kikao na waandishi wa habari jana Jumatatu nchini Marekani,
John Kerry ambaye wakati wa hotuba hiyo alikuwa pamoja na mwenzake wa
Ujerumani Frank-Walter Steinmeier, amesema amekubaliana na mwenzake wa
Russia, Sergei Lavrov juu ya kuunda ramani ya njia itakayohakikisha kuwa
mashambulizi ya vikosi vyao yanalenga tu matakfiri wa Daesh na
al-Nusra. Kerry amesema timu za mazungumzo za Geneva huko Uswisi ndizo
zitakazojadili kadhia hiyo ya kukiukwa makubaliano ya usitishaji vita.
Umoja wa Mataifa umesema makubaliano ya usitishaji vita yanatekelezwa
katika maeneo mengi ya Syria. Hata hivyo, Wizara ya Mambo ya Nje ya
Syria imesema kuwa Saudi Arabia inapanga njama ya kuvuruga makubaliano
hayo. Aidha Russia imeituhumu Uturuki kuwa imekiuka makubaliano hayo,
baada ya duru za habari kuripoti kuwa nchi hiyo ndiyo iliyohusika katika
hujuma ya hivi karibuni katika mkoa wa Latakia, kaskazini mwa Syria.
Wakati huo huo, serikali ya Moscow imesema kuwa, kufuatia mashauriano na mazungumzo ya kina, huenda chaguo la kuanzisha serikali ya kifederali nchini Syria likawa dawa mjarabu ya mgogoro wa Syria.
Katika kipindi cha karibu miaka mitano ya hujuma za magaidi Syria, takribani watu 470,000 wamepoteza maisha na mamilioni ya wengine kuachwa bila makazi.
K
Wakati huo huo, serikali ya Moscow imesema kuwa, kufuatia mashauriano na mazungumzo ya kina, huenda chaguo la kuanzisha serikali ya kifederali nchini Syria likawa dawa mjarabu ya mgogoro wa Syria.
Katika kipindi cha karibu miaka mitano ya hujuma za magaidi Syria, takribani watu 470,000 wamepoteza maisha na mamilioni ya wengine kuachwa bila makazi.
K
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269