Breaking News

Your Ad Spot

Mar 1, 2016

RAIS ALI BONGO KUWANIA URAIS NCHINI GABON

Rais Ali Bongo kuwania tena urais nchini Gabon
Rais wa Gabon Ali Bongo amesema atawania kuhifadhi kiti chake kwa muhula wa pili katika uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika baadaye mwaka huu.
Rais Bongo alitoa tangazo hilo jana Jumatatu alipolitembelea eneo lenye utajiri wa mafuta la Port Gentil, ambalo limekuwa likionekana kama ngome ya upinzani nchini humo. Katika hotuba yake hiyo, Rais wa Gabon alisema kuna haja ya kukabiliana na kile alichokitaja kuwa mfumo wa unyonyaji, ambapo watu wachache pekee ndio wenye kustafidi na utajiri wa mafuta wa nchi hiyo ya Afrika. Ali Bongo ambaye aliingia madarakani mwaka 2009 baada ya kifo cha baba yake, Omar Bongo ambaye aliitawala nchi hiyo tokea mwaka 1967; anatazmiwa kupata ushindani mkali kutoka kwa kiongozi wa upinzani Jean Ping, mwanadiplomasia maarufu wa Gabon ambaye alikuwa mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika kutoka mwaka 2008 hadi 2012. Wananchi wa Gabon wamekuwa wakifaya maandamano mara kwa mara, kulalamikia ugumu wa maisha na tuhuma za kukandamizwa viongozi wa upinzani na wakosoaji wa serikali.
Uchaguzi mkuu nchini Gabon unatazamiwa kufanyika mwezi Agosti mwaka huu, ingawa tarehe ya uchaguzi huo bado haijaainishwa na vyombo husika hadi sasa.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages