Breaking News

Your Ad Spot

Mar 1, 2016

LARIJANI : UCHAGUZI IRAN ISHARA YA KUSHINDWA MABEBERU

Larijani: Uchaguzi Iran ishara ya kushindwa mabeberu
Mkuu wa Vyombo vya Mahakama nchini Iran amesema kujitokeza kwa wingi wananchi wa Jamhuri ya Kiislamu katika uchaguzi wa Ijumaa iliyopita ni ithibati tosha kuwa taifa la Iran linatii miito ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu sambamba na kutuma ujumbe wa kufeli njama za mabeberu dhidi ya taifa hili.
Ayatullah Sadeq Amoli Larijani amewapongeza wananchi wa Iran kwa kushiriki kwa wingi katika uchaguzi wa Bunge la 10 la Jamhuri ya Kiislamu na wa 5 wa Baraza la Wanazuoni Wataalamu wanaomchagua Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu. Ayatullah Larijani amesema uchaguzi wa Februari 26 umetuma ujumbe kwa dunia kwamba taifa la Iran lingali linafungamana na mfumo wa Mapinduzi ya Kiislamu na miongozo ya Kiongozi Muadhamu, Ayatullah Ali Khamenei. Akiashiria propaganda zilizoenezwa kabla ya uchaguzi na vyombo vya habari vya Marekani na Uingereza, Mkuu wa Vyombo vya Mahakama nchini Iran amesema kuwa, taifa hili limeonyesha kuwa haliwezi kuhadaiwa na maadui wake ili kubadili misimamo yake.
Kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Iran, asilimia 62 ya wananchi milioni 55 waliotimiza masharti ya kupiga kura walishiriki katika uchaguzi huo wa Ijumaa iliyopita.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages