Breaking News

Your Ad Spot

Mar 19, 2016

MAZUNGUMZO YA MAWAZIRI WA MASHAURI YA KIGENI YA IRAN NA UTURUKI MJINI ISTANBUL

Mazungumzo ya Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni ya Iran na Uturuki mjini Istanbul
Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Uturuki wamekutana na kufanya mazungumzo mjini Istanbul na kujadili masuala ya uhusiano wa pande mbili, kieneo na kimataifa.
Dakta Muhammad Javad Zarif Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ambaye yuko nchini Uturuki kwa ziara rasmi amefanya mkutano wa pamoja na waandishi wa habari akiwa na mwenyeji wake, Mevlut Cavusoglu, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Uturuki. Dakta Zarif amesema, misimamo ya Iran na Uturuki kuhusiana na matukio ya Mashariki ya Kati inakaribiana sana na kwambva, Tehran na Ankara zinasisitiza juu ya kulindwa umoja wa ardhi ya Syria.
Waziri Zarif amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inapinga baadhi ya njama za kutaka kuigawa ardhi ya Syria na kuongeza kuwa, siasa za Tehran zimesimama juu ya msingi wa kuheshimu umoja na mamlaka ya nchi zingine.
Aidha Waziri wa Mashauri ya Kigeni ya Iran amelaani shambulio la kigaidi lililotokea leo katika mji wa Istanbul na kubainisha kwamba, shambulio hilo lililo dhidi ya ubinadamu limezidi kuonesha sura mbaya ya ugaidi.
Kwa upande wake Mevlut Cavusoglu, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Uturuki sambamba na kuashiria kwamba, Uturuki ina wakimbizi zaidi ya milioni tatu kutoka Syria amesema kuwa, Tehran na Ankara zitafanya hima ya kuhakikisha umoja wa ardhi ya Syria unahifadhiwa.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages