Breaking News

Your Ad Spot

Mar 1, 2016

WAZIRI WA SAUDIA ATEMBELEA ISRAEL KWA SIRI KUPANGA NJAMA DHIDI YA SYRIA

Waziri wa Saudia atembelea Israel kwa siri kupanga njama dhidi ya Syria
Saudi Arabia inashirikiana kikamilifu na utawala haramu wa Israel katika njama ya kuomuondoa marakani Rais Bashar al-Asad wa Syria pamoja na kuwepo mapatano ya usitishwaji vita nchini humo.
Imedokezwa kuwa viongozi wa ngazi za juu wa Saudi Arabia wametembelea Israel kwa siri katika kipindi cha siku chache zilizopita.
Shirika la Habari la Sputnik News la Russia liliandika Jumapili ya jana kuwa, Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia Adel Al Jubeir na Khalid Al Hamidan Mkuu wa Shirika la Ujasusi la Saudia wametembelea Israel kwa siri.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo wawili hao walikuwa na ujumbe maalumu wa kiusalama ambao ulihusu oparesheni za kijeshi dhidi ya Syria na Lebanon. Uamuzi huo ulichukuliwa katika mkutano wa maafisa wa ngazi za juu wa Saudia na wakuu wa utawala haramu wa Israeli akiwemo mkuu wa shirika la ujasusi la utawala huo, Mossad. Aidha imedokezwa kuwa katika safari hiyo ya siri, Al Jubeir pia amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni Benjamin Netanyahu.
Sputknik imefichua kuwa, lengo kuu la safari ya Adel Al Jubeir huko Israel ni ombi la Saudia kwa Israel kuingilia moja kwa moja kijeshi kusini mwa Syria kupitia hujuma ya nchi kavu ili kuishinikiza kijeshi Syria.
Gazeti la Financial Times la Uingereza pia wiki iliyopita liliripoti kuwa Saudi Arabia inataka kutekeleza hujuma ya kijeshi dhidi ya Syria kwa ushirikiano na Uturuki.
Watawala wa Saudia wangali wanafuatilia njama ya kumuondoa madarakani Rais Bashar al Assad wa Syria pasina kutumia njia za kisiasa na mazungumzo ya amani. Ni kwa msingi huo ndio maana utawala wa Kizayuni wa Israel ukaunga mkono njama hizo za Saudia kwa matumaini kuwa huo utakuwa mwanzo wa kusambaratika mstari wa mbele wa mapambano katika eneo la mashariki ya Kati. Tokea uanze mgogoro wa Syria, magaidi wanaopigana dhidi ya serikali ya Damascus wamekuwa wakipata matibabu katika hospitali za Israel zilizo katika eneo linalokaliwa kwa mabavu la Milima ya Golan.
Aidha maafisa wa jeshi la Israel wamekuwa wakiwapa mafunzo ya kijeshi magaidi wa makundi ya ISIS au Daesh na Jabhatu Nusra.
Kufichuka safari ya siri ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudia huko Israel pamoja na matamshi ya hivi karibuni ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani John Kerry kuwa iwapo usitishaji vita Syria utafeli basi kuna mpango mbadala ni mambo yanayoashiria kuwepo ushirikiano wa karibu kati ya Marekani, Israel na Saudia katika njama dhidi ya Syria. Ni wazi kuwa pande hizo tatu zinatekeleza njama za kumuondoa madarakani Rais Assad kwa kutumia njia zozote zinazowezekana.
Kumeibuka wasiwasi wa kutofanikiwa mapatano ya utekelezwaji mapatano ya usitisahji vita Syria kutokana na matamshi ya John Kerry. Hujuma ya kijeshi ni kati ya mpango mbadala wa Marekani iwapo utafeli mchakato wa kisiasa katika kutatua mgogoro wa Syria.
Weledi wa mambo wanasema katika safari yake ya siri Israel, Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudia alijadili na Wazayuni njia za kuwapa nguvu magaidi Syria katika kipindi hiki cha wiki mbili za usitishwaji vita.
Miaka mitano ya mgogoro wa Syria na kusimama kidete taifa la Syria na Rais Assad mbele ya njama za magaidi na waitifaki wao ni jambo linaloashiria kuwa, kumuangusha Assad si chaguo rahisi kwa Saudia, Uturuki na Israel

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages