Waziri Angella Kairuki |
NA IMMACULATE MAKILIKA- MAELEZO
Serikali
ya Tanzania yasifika kwa kuwa na uongozi unaozingatiaSheria na Utawala Bora.
Hayo
yamesemwa jijini Dar es Salaam na Waziri wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angella Kairuki alipokuwa akifungua
Mkutano wa siku mbili wa Kimataifa
kuhusu Utawala wa Sheria na Utawala bora.
Lengo
la mkutano huo ilikuwa ni kujadili
masuala ya Afrika katika kukuza utawala wa sheria katika utekelezaji wa agenda
ya maendeleo endelevu ya mwaka 2030 na agenda ya Umoja wa Afrika ya 2063.
“Mkutano
huu wa kistoria nchini Tanzania utasaidia kuleta mageuzi katika Taasisi
zinazosimamia masuala ya Sera na Sheria ambayo yatachochea maendeleo mazuri
katika nchi za Afrika”, alisema Waziri Kairuki.
Akiendelea
kuzungumza Waziri Kairuki alisema uwepo wa Marais wastaafu kama Mhe.Benjamin
Mkapa na Dkt. Jakaya Kikwete, katika mkutano huo ni ushahidi tosha wakuwepo na
mafanikio ya utawala wa sheria na utawala bora nchini Tanzania.
Kwa
upande wa Rais Mstaafu Mhe.Benjamin Mkapa, amesema ili Bara la Afrika liendelee
Kiuchumi ni lazima watu wake wapate elimu ya uraia ili waweze kushiriki zaidi
katika masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo yao pamoja na kuwepo na uongozi
utakaoleta mabadiliko “transformative leadership”.
Naye,
Waziri wa Haki Sudani ya Kusini Mhe. Pwanauwilla Unango amesema pamoja na kuwa
Bara la Afrika lina matatizo mengi kama vita, njaa, magonjwa na ndoa za
utotoni, dunia isiitazame Afrika kwa mtazamo huo pekee, bali inahitaji msaada
kutoka Jumuiya za Kimataifa.
Mkutano
huo wenye kauli mbiu “Kufikia agenda ya 2030 na agenda ya 2063:Utawala wa
Sheria kwa Maendeleo Endelevu ya Afrika”, (Achieving the 2030 agenda and agenda
2063:The rule of law as a driver of Africa’s suistainable development) ,
umeandaliwa na Shirika la Kimataifa la
Maendeleo ya Sheria (IDLO) la nchini Italia, kwa Ushirikiano wa Serikali ya
Tanzania umehusisha wadau mbalimbali
wakiwemo Mawaziri, kutoka nchi mbalimbali za Afrika, Mabalozi kutoka ndani na
nje ya Afrika pamoja na wawakilishi wa Mashirika ya kutetea Haki za Binadamu.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269