Wanawake zaidi ya 66,000 wa Marekani
wametangaza kuwa wapo tayari kushiriki katika maandamano makubwa
yaliyopangwa kufanyika Januari 21 mwakani, siku moja baada ya kuanza
kazi rais mteule wa nchi hiyo Donald Trump katika Ikulu ya White House.
Maandamano
hayo yaliyopewa jina la "Maandamano ya Wanawake Washington" yamewavutia
watu wengi kutoka pembe mbalimbali za Marekani. Wanawake wengine
156,000 tayari wamesema wapo tayari kushiriki kwenye maandamano hayo
mbali ya wale waliotangaza waziwazi kuwa watashiriki katika maandamano
hayo mjini Washington.
Maandamano
hayo ni sehemu ya ghasia ba maandamano yanayoshuhudiwa katika miji
mbalimbali ya Marekani baada ya Donald Trump kuibuka mshindi katika
uchaguzi wa Rais wa Marekani dhidi ya mpinzani wake Bi Hillary Clinton.
Wakati
huo huo Seneta Bernie Sanders wa chama cha Democrat amesema kuwa mtindo
wa Electoral College yaani kura za wajumbe wa majimbo 50 ya Marekani
unahitaji kuangaliwa upya baada ya kutangazwa tena mshindi mtu ambaye
hakupata kura nyingi za wananchi.
Akizungumza
katika mahojiano na jarida la USA Today, Seneta huyo wa Vermony amesema
kuwa ushindi aliopata rais mteule wa Marekani, Donald Trump kutoka
chama cha Republican dhidi ya mpinzani wake wa chama cha Democratic,
Hillary Clinton unazidisha ulazima wa kufanyika mjadala muhimu kuhusu
maana ya kura hizo za wajumbe wa majimbo 50 ya Marekani. Seneta Bernie
Sanders amesema:" kuna udharura wa kuangaliwa mfumo mzima wa Electoral
College ambao unampa madaraka ya nchi mtu ambaye hajapata kura nyingi za
wananchi. Amesisitiza kuwa jambo hili linahitaji mjadala mkubwa.
Kura za wajumbe hao wa majimbo 50 ya Marekani ndizo zinazompa ushindi
mgombea wa kiti cha urais na si kura za moja kwa moja za wananchi.
Itakumbukwa
kuwa, Hillary Clinton amepata kura nyingi zaidi ya mpinzani wake,
Donald Tramp katika uchaguzi wa hivi majuzi nchini Marekani lakini
Trump ametangazwa mshindi wa kiti cha rais kutokana na kupata kura
nyingi zaidi za Electoral College au wajumbe wa majimbo 50 ya Marekani
licha ya kupata kura chache zaidi zilizopigwa na wananchi.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269