Breaking News

Your Ad Spot

Nov 3, 2016

RAIS DUTERTE WA UFILIPINO: VIONGOZI WA MAREKANI NI WAPUMBAVU NA TUMBILI

Rais Rodrigo Duterte wa Ufilipino amewakosoa vikali viongozi wa Marekani kutokana na hatua yao ya kusimamisha muamala wa mauziano ya bunduki elfu 26 kwa nchi yake.
Rais Rodrigo Duterte amesema kuwa, viongozi wa Marekani waliochukua uamuzi wa usitishaji wa muamala huo ni wapumbavu na tumbili.  Katika hotuba yake hapo jana rais huyo wa Ufilipino aliwatoa wasi wasi raia wa nchi yake kwamba, kuna uwezekano serikali ya Manila ikaamua kununua silaha hizo za kijeshi kutoka Uchina au Urusi.
Mgogoro wa Marekani na Ufilipino
Alisema, "tayari China na Russia zimetualika na ziko tayari kututumia kiasi chochote cha silaha tunachohitajia." Mwisho wa kunukuu. Jumanne iliyopita, Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) ilitangaza kusitisha muamala wa mauziano hayo ya silaha kwa ajili ya polisi ya Ufilipino. Wizara ya Ulinzi ya Marekani ilidai kuwa, imechukua hatua hiyo kutokana na wasi wasi wake  juu ya vita dhidi ya magendo ya madawa ya kulevya vilivyotangazwa na Rais Rodrigo Duterte. Mvutano kati ya Washington na Manila umezidi kushtadi ambapo hivi karibuni rais wa Ufilipino alitangaza kukata mahusiano na Marekani.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages