Breaking News

Your Ad Spot

Nov 3, 2016

RIPOTI MPYA YA UFISADI WA KIFEDHA DHIDI YA RAIS JACOB ZUMA YAMUWEKA PABAYA

Taasisi ya kupambana na ufisadi wa kifedha nchini Afrika Kusini imetoa ripoti yake mpya kuhusiana na tuhuma za ufisadi zinazomkabili Rais Jacob Zuma wa nchi hiyo.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, kuna ulazima wa kufanyika uchunguzi wa kina kuhusiana na suala hilo. Rais Zuma alijitahidi sana kutohusishwa na ripoti hiyo ya ufisadi wa kifedha,  kiasi cha kumfanya wakili wake wa utetezi kujitoa kunako uamuzi huo. Saa chache baada ya kujiondoa huko, taasisi ya kupambana na ufisadi wa kifedha nchini humo ilitoa ripoti yake na hivyo kuchafua zaidi sura ya rais huyo katika fikra za walio wengi nchini.
Maandamano dhidi ya Rais Jacob Zuma
Sehemu ya ripoti hiyo yenye kurasa 355 inamuhusisha Rais Jacob Zuma na ufisadi mkubwa wa kifedha kati yake na familia moja ya Kihindi kwa jina la Gupta. Inaelezwa kuwa familia hiyo ya wafanyabiashara wa India, ina taathira kubwa kwenye serikali ya rais huyo, huku ikihusika pia katika uteuzi wa baadhi ya mawaziri wa serikali yake. Kufuatia ripoti hiyo, raia wengi wa Afrika Kusini walifanya maandamano hapo jana wakimtaka Rais Zuma ajiuzulu, ingawa polisi waliingilia kati na kuwatawanya.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages