Breaking News

Your Ad Spot

Jan 20, 2017

KINANA AWASHANGAA WAPINZAI KUDAI KUIBIWA KURA KILA UCHAGUZI

* Awataka wana CCM kutodharau chaguzi ndogo 
* Asema kudharau chaguzi hizo ni sawa na kudharau kesi 
*Unaiona ni ndogo unatahamaki umefungwa jela
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na makada ambao ni mawakala wa CCM katika uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Kijichi, Mbagala, Dar es Salaam, alipokuwa akifunga  semina ya mawakala hao, leo Janauari 20, 2017. Uchaguzi mdogo wa Unatarajiwa kufanyika Jumapili hii nchini kote.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisaini kitabu cha wageni alipopita kwenye ofisi ya CCM Kata ya Kijichi akiwa njiani kenda kufunga semina ya makada ambao ni mawakala wa CCM katika uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Kijichi, Mbagala, Dar es Salaam, leo Janauari 20, 2017. Kulia ni Mgombea wa Udiwani kwa tiketi ya CCM katika uchaguzi huo, Tausi Milanzi.
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiwsili ukumbini kwa ajili ya kufunga semina hiyo. Kulia ni Mgombea Udiwani katika kata ya Kijichi  Tausi Milanzi, Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida.
Mawakala wa CCM katika Uchaguzi mdogo wa Udiwani Kata ya Kijichi, Mbagala Dar es Salaam, wakimshangilia, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alipowasili ukumbini kufunga semina yao, leo
Meneja wa kampeni za CCM za uchaguzi mdogo wa Udiwani Kata ya Kijichi, Mbagala, Dar es Salaam, akitoa maelezo, kabla ya Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana kufunga semina ya mawakala wa CCM katika uchaguzi huo leo
Mgombea wa Udiwani kwa tiketi ya CCM, katika Uchaguzi Mdogo wa Madiwani, Kata ya Kijichi, Mbagala, Dar es Salaam, Tausi Milanzi, akisalimia mawakala wa CCM waliokuwa kwenye semina maalum, kwa ajili ya uchaguzi huo
Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga, akisalimia viongozi na mawakala wa CCM, katika Ucaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Kijichi
Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga, akisalimia viongozi na mawakala wa CCM, katika Ucaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Kijichi
Katibu Mkuu wa CCM, akipokea kadi kutoka kwa aliyekuwa mwanachama wa Chadema Adam Hamis ambaye aliamua kuhamia CCM, wakati wa Semina ya Mawakala wa CCM katika uchaguzi mdogo wa Udiwani Kata ya Kijiji, iliyofanyika leo
Kisha Katibu Mkuu akampa Kapelo rasmi ya CCM
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Temeke Yahya Sikunjema akimkaribisha Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, ili amkaribishe Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana kufunga semina hiyo
Mwenyekiti wa CCM mkkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida akifafanua jambo kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana kufunga semina hiyo
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na makada ambao ni mawakala wa CCM katika uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Kijichi, Mbagala, Dar es Salaam, alipokuwa akifunga  semina ya mawakala hao, leo Janauari 20, 2017. Uchaguzi mdogo wa Unatarajiwa kufanyika Jumapili hii nchini kote.
--------------
Na Bashir Nkoromo
Akifunga semina hiyo, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana aliwashangaa wapinzani kwamba kwa nini kila baada ya uchaguzi huwa wanalalamika kuwa wameibiwa kura.

"Zamani wakati mimi ni Mbunge, wakati wa uchaguzi, kura zilikuwa zinaenda kuhesabiwa wilayani, lakini siku hizi Mawakala wa vyama vyote wapo, walinzi wapo, tena kura zikishapigwa zinahesabiwa hapohapo kisha matokeo yanabandikwa ukutano hapohapo, wizi huo wa kura utatokea wapi?" alisema na kuhoji Kinana.

Kinana aliwaasa mawakala wa CCM katika uchaguzi huo mdogo wa Kijichi, kuhakikisha kila mmoja anatimiza waibu wake na kusema kwamba, anao uhakika ikiwa mawakala hao watafanya kazi zao vizuri basi CCM itashida.

"Ndugu zanguni, uchaguzi unazo sehemu nyingi, kuna kuteua wagombea, kupiga kampeni, na kupiga kura. sasa katika hatua zote hatua iliyokubwa zaidi ni hii ya kupiga kura, maana hapa ukiharibu umekosa kila kitu", alisema Kinana.

Alisema, japokuwa uchaguzi wa Udiwani katika kata hiyo ya Kijichi ni uchaguzi mdogo, lakini ni lazima kusimama kidete na kuhakikisha CCM nashinda tena kwa kishindo.

"Kweli huu ni uchaguzi mdogo, lakini nachotaka kuwaambia ni kwamba, uchaguzi ni kama kufanyiwa upasuaji, kama unafanyiwa upasuaji wataalam wanaweza kuuita mdogo, lakini wewe unayeenda kupasuliwa usiseme hivyo, ni kama vile kesi inayokukabili mahakamani, unaweza kuidharau ukatahamaki umefungwa, basi tusidharau kamwe uchaguzi huu", alisema, Kinana.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages