Waziri wa
Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu
akiongea na wadau wa Baraza la Wakunga hawapo pichani wakati
wa kuzindua mradi wa Mkunga Okoa Maisha kwa kushirikiana na watu wa
Canada.
Waziri wa
Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu (wa pili kushoto) akikata utepe kuashiria kuzindua mradi wa Mkunga Okoa Maisha ,
wa kwanza kushoto ni Balozi wa Canada Bi. Susan Steffan na wakawnza
kulia ni Katibu Mkuu wa Baraza la Wakunga nchini Dkt. Sebalda Leshabari.
Waziri wa
Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu ametoa
agizo kwa viongozi wote nchini kuacha mara moja kuwakamata wauguzi,
wakunga na kuwaweka ndani na badala yake wanapaswa kufuata taratibu
zilizopo.
Akizungumza
hayo wakati wa uzinduzi wa mradi wa Mkunga Okoa Maisha Waziri wa Afya
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu alisema
wakunga wanalo baraza ambako ndilo suluhishi la matatizo yao.
“Aidha
Mhe. Ummy amesema kuwa pale ambapo muuguzi au mkunga anapokosea zipo
taratibu za kufuata na siyo kumweka ndani kwani kuna Baraza la Wakunga
ambalo lina Mamlaka ya kisheria za kuchukua kwa mkunga yoyote ambaye
amekwenda kinyume.
“Tunao
Wakunga na wauguzi ambao wanafanya kazi zaidi ya masaa, tumeona
kilichotokea Sikonge, kiongozi anakuja juu kwanini mtoto amepewa dawa ya
Quinn,” alisema Ummy.
Kwa
upande wake Katibu Mkuu wa Baraza la Wakunga nchini Dkt. Sebalda
Leshabari amesema kuwa mradi huo unalenga kupunguza vifo katika Mikoa
ya Shinyanga na Simiyu hivyo wauguzi na wakunga ni vema wakashirikiana
na Baraza hilo ili kufanikisha malengo yao.
WIZARA YA AFYA.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269