Breaking News

Your Ad Spot

Jun 14, 2014

NHIF WAENDELEA KUSAIDIA HUDUMA KWENYE WODI YA AKINA MAMA NA WATOTO KITUO CHA AFYA MLANDIZI

 Mwenyekiti wa kamati ya kituo cha afya Mlandizi, bw Makamba Mwaluka (watatu kushoto), akiwakaribisha wageni kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya baada ya kufanya ziara katika wodi ya akina mama na watoto Kituo cha Afya Wilayani Mlandizi. Juni 12,2014 na kukabidhi mashuka kwenye kituo hicho (kulia kwake), Muendeshaji shughuli mama Gaudensia Ndegea (katikati kulia), Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha, Michael John, na Mjumbe wa bodi NHIF, bwana Charlse Kajege.  
 Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa NHIF, Raphael Mwamoto (kulia), akiwakaribisha wageni aliyoambatana nao kutoka katika mfuko huo(wakwanza kulia), Mjumbe wa bodi NHIF, Charlse Kajege, Mjumbe wa bodi wa NHIF Dr. Hashim Mohamed, Diwani wa Mlandizi  mama Ndessi, Mkurugenzi wa Matibabu na Huduma za kiufundi  Dr. Frank Lekey
 Mjumbe wa bodi wa NHIF Dr. Hashim Mohamed(kushoto), akikabidhi mashuka kwa mgeni rasmi, diwani wa Mlandizi  mama Ndessi baada ya kufanya ziara katika katika wodi ya akina mama na watoto Kituo cha Afya Wilayani Mlandizi na kukabidhi mashuka kwenye kituo hicho.
 Mjumbe wa bodi aliyemuwakilisha Mwenyekiti wa bodi ya NHIF Dr. Hashim Mohamed (katikati), akisisitiza jambo mara baada ya kumaliza ziara hiyo wilayani Mlandizi.
 Wajumbe wa bodi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ndugu Charlse Kajege na Dr. Mohamed Hashim wakiwa na diwani wa Mlandizi Mama Dessi       wakitandika moja ya mashuka yaliyotolewa na NHIF.katika wodi ya akina mama na watoto Kituo cha Afya Wilayani Mlandizi.
Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti,Raphael Mwamoto(kushoto), akimtambulisha Mkurugenzi wa huduma za utabibu na ufundi  Dr. Frank Lekey ambaye waliambatana katika ziara hiyo wilayani mlandizi.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages