Breaking News

Your Ad Spot

May 7, 2015

MIPANGO YA SERA ZITEKELEZWE KUMUOKOA MAMA NA MTOTO MCHANGA

DSC_0334
Mratibu wa Mawasiliano na uhamisishaji wa mradi wa Mama Ye unaoendeshwa na asasi ya Evidence for Action linalofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Uingereza (DFID), Chiku Lweno akielezea jitihada zinazofanywa na mradi wa Mama Ye katika kukabiliana na vifo vya Mama na mtoto ambapo aliwataka waandishi wa habari kutumia kalamu zao kuelemisha jamii ili iweze kuepukana na vifo vya mama na mtoto ambalo nalo ni janga la taifa.(Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog).

Na Mwandishi wetu, Musoma
SERIKALI imeshauriwa kuhakikisha sera na mipango mizuri iliyopo kwa afya ya mama na mtoto mchanga inasimamiwa na kutekelezwa ili kuliondoa taifa katika janga la kupoteza mama na watoto wakati wa uzazi.

Kauli hiyo imetolewa na Mratibu wa Mawasiliano na uhamisishaji wa mradi wa Mama ye unaoendeshwa na asasi ya Evidence for Action linalofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Uingereza (DFID),  Chiku Lweno katika  mafunzo kwa waandishi wa habari mjini Musoma.

Alisema bila kutekeleza mipango mizuri ambayo Rais Jakaya Kikwete amekuwa championi wa masuala ya wanawake na watoto kitaifa na mataifa, tatizo la vifo kwa wanawake wenye pingamizi za uzazi na watoto wachanga.

Alisema kutokana na haja ya  kutoa msukumo katika masuala ya uzazi wameamua kuwapatia elimu waandishi wa habari ili wawe chachu ya kutambua umuhimu wa ukunga na uzazi salama.

"Tunafunza waandishi wa habari  ili waweze kusukuma mbele shahuri hili ili kila mtu katika nafasi yake atetee nafasi yake" alisema Lweno.

Alisema suala la mama na mtoto mchanga ni masuala mtambuka ambapo mambo mengi lazima yaunganishwe yafikiriwe na kutambuliwa  ili kudhibiti vifo vya wanawake na watoto wachanga.

Alitaja masuala hayo kama upangaji wa bajeti ya kueleweka kwa ajili ya kusaidia kupatikana kwa wakunga wataalamu na vifaa vyao vya kazi na maeneo ya kufanyia kazi. Aidha kuwapo kwa ukubali wa wakunga na elimu ya uzazi.

Alisema ni vyema waandishi wa habari kama watia chachu kuelimishwa mambo mengi yanayohusiana na uzazi salama ambapo ndani yake kuna masuala ya bajeti na ufuaji wa wataalamu na ufuatuiliaji wa sera na sheria zilizopo katika kuhakikisha usalama wa mama na mtoto.

Alisema  anaamini waandishi wa habari wakielewa mambo hayo watasaidia kukomaa nalo na kuwezesha kila mtu kuwajibika.
DSC_0278
Kaimu Muuguzi Mkuu wa Serikali kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Ama Kasangala akifafanua jambo kwa washiriki wa mafunzo ya siku moja yaliyofadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu (UNFPA) kuelekea kwenye kilele cha sherehe za maadhimisho ya siku ya wakunga duniani ambapo kitaifa imefanyika mkoani Mara.
Naye Afisa Muuguzi mwandamizi kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii, Saturini Manangwa akiwasilisha mada kwa waandishi wa habari alisisitiza haja za waandishi kutambua dhana ya afya ya mama na mtoto kuwa ni kitu mtambuka kutokana na suala la lenyewe kutegemeana.

Alisema serikali inapohimizwa kuwekeza kwa mkunga  kunatokana na ukweli kuwa huduma ya mama na mtoto mchanga itakujwa bora kwa kuwa na mkunga  bora mwenye vifaa na anayefahamu wajibu wake kuanzia ujauzito wa mama hadi kujifungua kwake.

Alisema uwekezaji huo unagusia  changamoto nyingi zilizopo sasa kama upungufu wa wakunga, vituo vya kutolea huduma, dawa, miundombinu na masuala anuai ambayo yameegemezwa na utambuzi wa bajeti na umuhimu wake kama kipaumbele.

Alisema kwamba katika upangaji bajeti kila kitu kinategemea huwezi kusema unazidisha hiki na unakiacha hiki.
Alisema mathalani katika hali bora ya ukunga na uwezo wa kumsaidia mhusika ,viwango vya dunia vilivyoweka na Shirika la Afya Duniani (WHO)  kila mkunga mmoja ahudumie angalau watu sita, lakini sehemu kubwa ya dunia haifikii hivyo.

Aidha alisema kwa Tanzania kiwango ni mkunga mmoja ahudumie watu 20-25 lakini kwa sasa Tanzania mkunga mmoja anahudumia zaidi ya watu 50.

 Kimsingi alisema Tanzania ina tatizo la wakunga na pamoja na serikali kuanzisha vyuo vya kufunza wakunga na kukubali mashirika ya dini nayo kufanya hivyo hali bado ni tete.

Hata hivyo alisema ni kupitia wakunga waliowataalamu  upo uwezekano wa kuzuia vifo visivyo vya lazima.
DSC_0253
Mratibu wa Chama cha Wakunga nchini (TAMA), Martha Rimoy akizungumzia nia ya chama hicho ni kuhakikisha kwamba kila mwanamke mwenye uwezo wa kuzaa anapata huduma za mkunga mtaalamu.

Muuguzi huyo mwandamizi pia alisema katika juhudi za serikali kunaanzishwa mafunzo ya mwaka mmoja ambapo yatatoa maofisa afya ambao kazi yao kubwa itakuwa kujua idadi ya wanawake wajawazito na wagonjwa katika maeneo yao na kutoa taarifa kwa zahanati iliyo karibu.

Alisema ofisa huyo kazi yake haitakuwa hospitalini au kwenye zahanati bali kwenye jamii akitambua idadi ya wagonjwa wake na kutoa taarifa sahihi ya hali ya afya ya kitongoji chake kwenye zahanati.

Mmoja wa washiriki  Belina Nyakeke ambaye  ni mwandishi wa habari wa magazeti alisema kwamba amefurahishwa na mafunzo hayo ambayo yamempa nafasi ya kutambua wajibu wake katika kusaidia kuondoa tatizo la vifo vya mama na mtoto mchanga.

Alisema japokuwa mafunzo ni ya muda mfupi lakini yamemfumbua macho kutambua wajibu na haki kwa wananchi na serikali.

Naye Ahmed Makongo akizungumzia mafunzo hayo alisema yamemfanya atambue wajibu wake kusaidia kusukuma mambo yaende sawa kwa upande wa waamuzi na pia wananchi husika kwa kuzingatia mafunzo hayo yaliyoletwa kwao na Mama Ye na UTTPC chini ya Ufadhili wa Shirika la Mpango wa watu Duniani (UNFPA).
DSC_0219
Ofisa muuguzi mwandamizi kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Saturini Manangwa akizungumza changamoto za upungufu wa wakunga, vituo vya kutolea huduma, dawa, miundombinu n.k wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari wa mjini Musoma mkoani Mara.
DSC_0299
Ofisa wa Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu (UNFPA) anayeshugulikia mifumo ya Afya, Felista Bwana akitoa takwimu za nchi zinazoongoza kwa vifo vya mama na mtoto kwenye mafunzo ya waandishi wa habari mjini Musoma. 
DSC_0244
Mwandishi wa habari wa gazeti la The Citizen, mkoani Mara, Belina Nyakeke (katikati) akishiriki kwenye mafunzo ya waandishi wa habari yaliyofanyika mjini Musoma na kufadhiliwa na Shirika la UNFPA.
DSC_0207
Mwandishi wa habari wa gazeti la Tanzania Daima mjini Musoma, Igenga Mtatiro akiuliza swali kwa Afisa muuguzi mwandamizi kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Saturini Manangwa (hayupo pichani).
DSC_0229
Pichani juu na chini ni baadhi ya waandishi wa habari wa mkoani Mara ambao pia wanachama wa vilabu vya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) walioshiriki mafunzo hayo yaliyoratibiwa na Mradi wa Mama Ye kwa kushirikiana na UTPC na kufadhiliwa na UNFPA.
DSC_0267
DSC_0260
DSC_0197
Rais wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya akisisitiza jambo kwa washiriki wa mafunzo hayo.
DSC_0242
Rais wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya (kushoto), akibadilishana mawazo na Mratibu wa Chama cha Wakunga nchini (TAMA), Martha Rimoy mara baada ya kuhitimisha mafunzo hayo.

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Seif Rashid afungua semina ya Waandishi wa Habari kuhusu Usalama wa Chakula katika kuadhimisha Siku ya Afya Duniani jijini Dar es Salaam

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid (kushoto), akihutubia wakati akiifungua semina ya siku moja ya waandishi wa habari kuhusu usalama wa Chakula katika kuadhimisha Siku ya Afya Duniani, jijini Dar es Salaam leo asubuhi. Kulia ni Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), nchini Tanzania, Dk. Rufaro Chatora.
Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), nchini Tanzania, Dk. Rufaro Chatora akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina hiyo. Kushoto ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Donan Mmbando (kushoto), akizungumza katika ufunguzi wa semina hiyo.
Mkuu wa kitengo cha usalama wa  chakula  maji na usafi wa mazingira wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Stephen Kiberiti akitoa mada kuhusu rasimu ya sera ya taifa ya chakula salama  na bora katika semina hiyo.
Mkurugenzi Msaidizi Elimu ya Afya kwa Umma, Helen Semu (kushoto), akiteta jambo na Mkurugenzi wa Usalama wa Chakula kutoka Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Raymond Wigenge wakati wa semina hiyo. Wakurugenzi hao walikuwa watoa mada katika semina hiyo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Donan Mmbando (kulia), akiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Kinga ... wa wizara hiyo, Dk.Georgina Msemo wakati wa ufunguzi wa semina hiyo.
 Wanahabari wakiwa kwenye semina hiyo.

Wanahabari wakichukua taarifa wakati wa ufunguzi wa semina hiyo.
Mkurugenzi wa Usalama wa Chakula kutoka Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Raymond Wigenge (kushoto), akielekezana  jambo na Ofisa Afya Muelimishaji wa Wizara hiyo, Aggrey Mshana wakati wa Semina hiyo.
(Imeandaliwa na Dotto Mwaibale)

Uzinduzi wa Huduma Mpya ya MaxMalipo kwa kutumia Simu ya Kiganjani

Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa kampuni ya MaxCom Africa Bw. Deogratius Lazari akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam kuhusu Huduma Mpya ya MaxMalipo  kwa kutumia simu ya kiganjani ijulikanayo kama SmartMalipo. Kushoto ni Afisa wa MaxCom Bw. Geofrey Mwakamyanda na kulia ni Meneja wa MaxCom Kanda ya Mashariki Bw. Thomas Mwakalindile. (Picha na Idara ya Habari-Maelezo)

MAXCOM Africa maarufu kama MaxMalipo ni kampuni ya Kitanzania iliyoanzishwa mwaka 2010 ambayo imewekeza katika kurahisisha maisha ya Watanzania na Waafrika kwa ujumla kiuchumi na kijamii kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya mawasiliano (ICT Technology)

Ili kufikia malengo na Sera ya Taifa ya kutumia mifumo ya kielekroniki kutoa huduma na pia kuwezesha Watanzania walio wengi kufikiwa na huduma hizi (Financial Inclusion)  na pia  kurahisisha ukusanyaji wa kodi na kuongeza ajira, MaxMalipo imeanzisha huduma  mpya itakayomuwezesha mtanzania kulipa bili zote kwa kutumia simu ya kiganjani  aina ya  Smart phone yenye Mfumo utakaojulikana kama SmartMalipo.

Huduma hii inatarajiwa kutoa ajira kwa watanzania takribani laki mbili (200,000)  nchi nzima kufikia mwaka 2016  na hivyo kuchangia ukuaji wa sekta isiyo rasmi ya ajira na kunyanyua uchumi wa Nchi.  Mfumo huu utaweza kurahisisha ulipaji wa bili mbalimbali Mfano; Umeme (Luku), Ving’amuzi vya Televisheni, Vocha za Mitandao yote, Kulipia Kodi za TRA na Baadae Kufanya Miamala ya Kibenki  inayohusisha Kuweka na Kutoa fedha, huduma ambazo kwa sasa zinalipwa kupitia mashine za MaxMalipo.

Huduma hiyo inapatikana kwenye mfumo wa simu ya kiganjani ambapo mtumiaji atalazimika kuweka  mfumo wa SmartMalipo (Download Smart Wakala Application) kutoka tovuti ya Google play au tovuti ya Maxmalipo kwa  kuandika neno ‘SmartMalipo  au Maxmalipo’. Kisha mtumiaji atapata maelekezo ya  jinsi ya ku-install mfumo huu kwenye simu yake na jinsi ya kutumia. Mfumo huu utamwezesha mtumiaji yeyote kuwa Wakala na kulipia huduma zilizo orodheshwa.

Mtumiaji  wa  mfumo huu  atajipatia kamisheni kama alivyo wakala mwingine wa Maxmalipo kwa Huduma atakazofanya. 

Watumiaji wa mfumo huu wa SmartMalipo watatambulika kwa jina la ‘Smart Wakala’ popote walipo na kufanya biashara kupitia simu zao za kiganjani.

MaxMalipo imeanzisha huduma hii mpya kwa lengo la kuwawezesha watanzania walio wengi kufikiwa zaidi na  huduma za malipo kwa haraka wakiwemo wafanyabiashara wadogo na wenye mitaji midogo  ambao kwa mazingira yao ni vigumu kuwa na Mashine za Maxmalipo. 

 MaxMalipo imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kupunguza matatizo ya foleni kwenye malipo ya huduma mbalimbali kama bili za TRA, LUKU, DAWASCO, huduma za kibenki na hata katika mifuko ya Hifadhi ya jamii Mfano PSPF.


Mwisho kampuni ya Maxcom Africa - Maxmalipo inatoa rai kwa watanzania hasa wafanyabiashara  kuchangamkia huduma zinazotolewa na kampuni hii ili kuendana na kasi ya maendeleo ya teknolojia katika mifumo ya utoaji huduma.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages