Katibu Mkuu wa
Baraza la Wanawake
Chadema Taifa BAWACHA na Mbunge Viti Maalumu Taifa Grace Tendega
(katikati) jana February 20,2016 akizindua ofisi Mpya ya Mbunge wa Viti
Maalumu Mkoa wa Mwanza Chadema, Susan Masele (Kulia). Kushoto ni
Paschazia Renatus ambae ni Katibu wa Bawacha Mkoa wa Mwanza.
Akizungumza katika
Uzinduzi huo, Tendega alipongeza uwepo wa ofisi hiyo ambayo itakuwa
ikisikiliza kero za wananchi bila kujalisha itikadi zao za kisiasa kwa
ajili ya kupokea hoja za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi ikiwemo
kuzisemea bungeni.
"...Kazi ya Mbunge
siyo kugawa hela. Kazi ya Mbunge ni kusikiliza kero za wananchi na
kuzitatua. Na mimi niseme nitakuwa mwakilishi bora na hapa tumeanza tu
ambapo katika ofisi hii nitakuwa napokea na kusikiliza kero za wananchi
na kwenda kuzisemea bungeni... Alisema Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa
Mwanza Chadema, Susan Masele.
Ofisi hiyo inapatikana Mtaa wa Ghana Green View, Kata ya Nyamanoro, Jimbo la Ilemela Mkoani Mwanza. Ndani yake pia kuna Ofisi ya BAWACHA Mkoa wa Mwanza.
Ofisi hiyo inapatikana Mtaa wa Ghana Green View, Kata ya Nyamanoro, Jimbo la Ilemela Mkoani Mwanza. Ndani yake pia kuna Ofisi ya BAWACHA Mkoa wa Mwanza.
Katibu
Mkuu wa Baraza la Wanawake Chadema Taifa BAWACHA na Mbunge Viti Maalumu
Taifa Grace Tendega (katikati) jana February 20,2016 akizindua ofisi
Mpya ya Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mwanza Chadema, Susan Masele. Kushoto ni Paschazia Renatus ambae ni Katibu wa Bawacha Mkoa wa Mwanza.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269