Breaking News

Your Ad Spot

Nov 2, 2016

TANGAZO LA BALFOUR; CHANZO CHA UKOSEFU WA AMANI MASHARIKI YA KATI

Matatizo yote ya kiusalama yaliyopo hivi sasa katika eneo nyeti la Mashariki ya Kati yanatokana na tangazo la Balfour.
Miaka 99 iliyopita, dola la kikoloni la Uingereza ilitoa tangazo la Balfour tarehe pili Novemba 1917. Arthur James Balfour, ndiye aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza wakati huo. Balfour alisoma tangazo hilo mbele ya Baron Walter Rothschild mkuu wa jamii ya Mayahudi wa Uingereza aliyekuwa pia mbunge wa nchi hiyio. Tangazo la Balfour lilikuwa na nafasi kubwa katika kuasisiwa mfumo maalumu wa kiusalama kwenye eneo la magharibi mwa Asia. 
Tangazo hilo lilikuwa batili tangu siku yake ya mwanzo kabisa kwani serikali ya Uingereza ililitumia kuasisi dola pandikizi la Kizayuni linaloitwa Israel katika ardhi ya nchi nyingine wakati hakuna sheria yoyote iliyoipa haki hiyo. Tangazo hilo ndio uliokuwa msingi wa kuundwa Israel mwaka 1948 katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu hadi leo hii, na tangu wakati huo, ukaanza mgogoro wa Palestina na eneo zima la Mashariki ya Kati bali ulimwengu mzima wa Kiislamu. Hadi hivi sasa mgogoro huo uliotokana na tangazo la mwezi Novemba 1917 la Balfour umeshasababisha vita visivyopungua vinane baina ya Israel na nchi za Karabu. Vita vingi zaidi kati ya hivyo ni vile vilivyotokea baina ya Israel na Lebanon na Israel na Palestina. Vita vya miaka ya 1948, 1956, 1967, 1972, 2006, 2008, 2012 na vita vya mwaka juzi 2014 ni miongoni mwa vita vikubwa zaidi vilivyotokea baina ya utawala pandikizi wa Israel na nchi za Kiarabu.
Bendera ya utawala mchakavu wa Israel

Fauka ya hayo, hadi hivi sasa Israel imeshafanya makumi ya mashambulizi ya muda mfupi na ya hapa na pale dhidi ya Lebanon na dhidi ya maeneo machache yaliyobakia mikononi mwa Wapalestina, kama ambavyo kumeshafanyika Intifadha tatu hadi hivi sasa za kupambana na Wazayuni. Intifadha ya kwanza ni ile iliyoanza mwaka 1978 na kumalizika mwaka 1993, yaani baada ya miaka 15 ya kuanza kwake. Intifadha ya pili ilianza mwaka 2000 na kuendelea hadi mwaka 2005, na Itifadha ya tatu ya Wapalestina ilianza mwezi Oktoba mwaka jana 2015 na ingali inaendelea hadi hivi sasa.
Matokeo ya mashambulizi, vita na Intifadha zote hizo ni kuuawa na kujeruhiwa pamoja na kuwa wakimbizi mamilioni ya raia Waarabu, nje na ndani ya ardhi za Palestina. Matokeo ya jambo hilo ni kuongezeka umaskini, ukosefu wa kazi, ukosefu wa utulivu na majanga mengine mengi katika eneo hili la magharibi mwa Asia.
Kuasisiwa utawala pandikizi wa Israel mwaka 1948 baada ya tangazo la Balfour la 1917


Zaidi ya hayo, Israel ndiyo nembo kuu ya ugaidi wa kiserikali na imekuwa ikiua watu muhimu wa ulimwengu wa Kiislamu katika maeneo tofauti duniani. Utawala wa Kizayuni wa Israel ndiyo sababu kuu ya uingilia wa madola ya Magharibi katika masuala ya ndani ya nchi za eneo hili. Ni jambo lisilo na shaka kuwa, uingiliaji wa mambo ya ndani ya nchi nyingine ni miongoni mwa mambo yanayoongeza ukosefu wa amani na utulivu na kuzusha mizozo baina ya nchi za eneo husika. Si hayo tu, lakini pia utawala wa Kizayuni wa Israel ni moja ya wavunjaji wakuu wa haki za binadamu duniani.
Utawala ambao unapora maeneo ya Wapalestina na kujenga vitongoji vya walowezi wa Kizayuni. Bila ya shaka ni kwa kuzingatia hali hiyo ndio maana tunaweza kusema kuwa, Tangazo la Balfour ndilo chimbuko na chanzo cha ukosefu wa amani na usalama katika eneo la Mashariki ya Kati, na kwa mara nyingine tena, mkoloni kizee Uingereza, ndiye muhusika wa mabalaa na majakamoyo yote haya. 

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages