Breaking News

Your Ad Spot

Nov 3, 2016

TAREHE 13 ABAN, NEMBO YA KUENDELEA MAPAMBANO YA WAIRANI DHIDI YA MAREKANI

Wananchi wa matabaka mbali mbali Iran wakiwemo wanachuo na wanafunzi leo Tarehe 13 Aban inayosadifiana na Novemba 3 wameandamana mjini Tehran na kote nchini Iran ya Kiislamu na kuonyesha uewepo mpana wa ujumbe wa kweli na wenye taathira wa Mapinduzi ya Kiislamu dhidi ya madola ya Kiistikbari hasa Marekani.
Maandamano ya Siku ya Kitaifa ya Kupambana na Uistikbari wa Kimataifa yamefanyika kote nchini leo Alhamisi na kuonyesha umoja baina ya kizazi cha zamani na kizazi kipya na wote kwa sauti moja wameonyesha kuchukizwa na uistikbari wa kimataifa kwa kupiga nara za 'Mauti kwa Marekani' na 'Mauti kwa Israel'.
Maandamano hayo yameonysha kuwa,  watu wa Iran, sawa na miaka 37 iliyopita, wanafahamu kikamilifu kuhusu njama za Marekani dhidi ya Iran na kwamba hawaliamini dola  hilo la kibeberu. Tarehe 4 Novemba mwaka 1979, wanafunzi wa Iran katika kulalamikia njama za Marekani dhidi ya Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran walivamia na kuzingira 'Pango la Ujasusi' (Ubalozi wa Marekani) mjini Tehran kwa lengo la kuzuia dola hilo la kibeberu kufikia malengo yake haramu dhidi ya mapinduzi machanga yaliyokuwa yamefikia ushindi Februari mwaka huo.
Wanafunzi Wairani walipoteka Pango la Ujasusi la Marekani, Tehran Novemba 4 1979
Nyaraka zilizofichuliwa katika Pango la Ujasusi zilithibitisha kuwepo uadui na njama kubwa za Marekani dhidi ya taifa la Iran.
Njama hizo zinaendelea hadi leo kwa njia mbali mbali na hata baada  ya vijana wanamapinduzi na wabunifu kuteka Pango la Ujasusi, lakini adui angali anaendeleza njama zake. Kwa msingi huo kizazi cha vijana wanamapinduzi hivi leo kina ufahamu wa kina zaidi kuhusu uadui wa Marekani dhidi ya Iran na hivyo vijana hao wamechukua hatua za kuzuia njama zaidi za dola hilo la kibeberu.
Ubunifu wa vijana wa Iran katika kuteka Pango la Ujasusi mjini Tehran ulikuwa na taathira kubwa kiasi cha Imam Khomeini MA kuutaja ubunifu huo kuwa, 'Mapinduzi ya Pili'.
Kauli hii ya  Mwasisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilitokana na kina cha njama na ukhabithi wa Marekani wakati wa Ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu na baada ya hapo. Punde baada ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu, dola la kiistikbari la Marekani lilianza kutekeleza njama dhidi ya mapinduzi haya ya watu wa Iran. Lakini kutokana na uangalifu pamoja na mwamko wa watu wa Iran, njama hizo zilisambaratishwa.
Kama alivyosema Ayatullah Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, kutekwa Pango la Ujasusi kulikuwa ni jibu muafaka la wananchi dhidi ya uadui wa dola la Marekani linalojitakia makuu ambalo kwa miaka mingi lilikuwa likipora utajiri wa Iran lakini mikono yake ikakatwa kufuatia ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
Kwa maneneo mengine ni kuwa, kutekwa Pango la Ujasusi la Marekani Tehran kulikuwa ni mwisho wa satwa yake nchini hapa. Jambo hilo linaonyesha wazi kwamba madola makubwa kama Marekani yatafeli katika njama zao dhidi ya Iran. Kuendelea uadui wa serikali mbali mbali za Marekani dhidi ya Iran kunatokana na kuendelea moyo wa hasira na chuki dhidi ya Marekani miongoni mwa wananchi wanamapinduzi wa Iran.
Maandamano dhidi ya Marekani, Tehran, Novemba 3 2016
Kusimama kidete Imam Khomeini MA mbele ya Marekani na pia kauli yake aliposema, "Pigeni Makelele Mnazoweza Dhidi ya Marekani" ni ishara ya ufahamu wake wa kina kuhusu uadui wa Marekani dhidi  ya Iran na hilo limethibitika katika historia.
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Khamenei amesema kuvunja Marekani ahadi zake katika mapatano ya nyuklia ni misdaki ya wazi ya kuendele uadui wake dhidi ya Iran. Amesisitiza kuwa, njia muhimu zaidi ya kustawi nchi si katika kufanya mazungumzo au kujikurubisha na Marekani bali ni kutegemea uwezo wa vijana ndani ya nchi na kuwa macho mbele ya sera hasimu za Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Katika taarifa ya mwisho wa maandamano ya Tarehe 13 Aban Alhamisi hii, washiriki wamesema hatua ya wananchi wa Iran ya kupinga dhulma na uistikbari imetokana na misingi ya Qur'ani Tukufu na mtazamo wa kimantiki. Aidha washiriki wamesema wataendelea na mkondo huo kwa kufuata miongozo ya Imam Khomeini MA na pia kwa kutii amri zenye hekima za Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu mbele ya uistikbari wa kimataifa.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages